Monday, July 2, 2012

MGOLO/ MJIKO/ HEMORRHOIDS



UTANGULIZI
Mgolo au kwa kimombo Hemorrhoids hutokea pale ambapo aina ya mishipa midogo Iitwayo vein iliyopo eneo la mwisho la Utumbo mkubwa liitwalo kwa ligha ya kimombo Rectum Kuvimba ama kujaa. Hali hii hutokea pale ambapo kani ya mgandamizo inapoongezeka ndani yake, mara nyingi kwa sababu ya kujikamua sana wakati wa kwenda Haja kubwa, pia huwapata wajawzito kwasababu ya kani ya mkandamizo ndani iletwayo na Ukubwa wa Tumbo la uzazi na jinsi linavyoongezeka.

AINA ZA MGOLO
Zipo aina mbili za mgolo ambazo zimepewa majina yake na kutofautishwa kwa sababu ya maeneo zinapojitokeza na Dalili zake.

MGOLO WA NDANI (INTERNAL HEMORRHOIDS)
Mgolo wa ndani (Internal haemorrhoids) hutokea ndani ya kuta za Rectum eneo la Utumbo mkubwa lililopo chini mwisho kabisa na huwa na mtu huwa hawezi kuzihisi uwepo wake, Mara zote huwa hazileti maumivu ile uwepo wake utagundua pale ambapo mtu hutokwa na  Damu wakati wa kupata Haja kubwa damu hii huchanganyika na choo kikubwa au mara nyingine hutangulia Damu.

MGOLO WA NJE (EXTERNAL HEMORRHOIDS)
Mgolo wa nje (External haemorrhoids) hujitokeza chini ya ngozi inayozunguka eneo lakutolea haja kubwa kimombo Anus. Hizi unaweza kuzishika na hata kuhisi uwepo wake zinapokuwa simejaa na wakati mwingine husababisha Muwasho ama Maumivu au hata kutokwa na Damu wakati wa kupata Haja kubwa. Mgolo wa nje hutokea na Kuleta Maumivu Makali pale ambapo Damu hujaa na kuganda ndani ya mishipa Midogo itwayo Kimombo Vieins



VISABABISHI VYA MGOLO
Mgolo huambatana na 1.Hali ya Kupata Choo Kigumu kwa kimombo tunaita constipation na pia hali ya kujikamua Unapokwenda Haja.  2.Ujauzito Pia hupelekea kutokea kwa Mgolo, Hali hizi husababisha kuongezeka kwa kani ya mkandamizo ndani ya mishipa midogo iliyopo eneo la Rectum iitwayo kwa lugha ya kimombo Hemorrhoidal Viens na kuifanya ijae na kuvimba. Visababishi vingine ni kama mfano Magonjwa Sugu ya Ini (Chronic LiverDisease). Mgolo ni Tatizo lililozoeleka sana kwasasa na linakadiliwa kutokea kwa zaidi ya nusu ya watu wenye umri wa kati ya miaka 50 Hamsini

DALILI ZA MGOLO
Dalili kubwa ni 1. kutokwa na Damu katika eneo la Haja kubwa pasipo maumivu yoyote. 2. Kupata Choo kikubwa chenye Damu 3. Damu kwenye Toilet Paper. 4. Muwasho eneo la haja kubwa na kukufanya ujisikie hali ya kutaka kwenda Haja kubwa Muda wote. Kutokwa Damu unapokwenda Haja kubwa si jambo la kulichukulia kirahisi au kawaida Hivyo unapopatwa na dalili hii unashauriwa kwenda kituo cha Afya Kwa Uchunguzi wa kitabibu. Ijapokuwa Mgolo ni moja ya sababisho kubwa la Kutokwa Damu wakati wa kupata Haja kubwa kunaweza kuwa bado na visababishi vingine kama Uvimbe, Maambukizi kwenye njia ya haja kubwa NK. 

MGOLO WA NDANI ULIO JITOKEZA NJE.
Hii hutokea pale ambapo Mgolo wa ndani Unapovimba sana na kujaa kisha hushuka taratibu kutoka eneo Ulipoanzia mpaka Kutoka nje ya njia ya haja Kubwa. can be felt as a lump outside the anus;
·         Upo uwezekano wa kuuludisha ndani taratibu ijapokuwa hii hitakuwa jawabu la kudumu nikiwa na maana kuwa tatizo laweza kijitokeza tena.
  • Mgolo uliotoka nje Unaweza kujaa zaidi kama hautarudishwa kwa wakati.
MGOLO WA NJE ULIOPATWA NA DAMU KUGANDIA
      MGOLO uliotokewa na mgando wa Damu ndani yake Huleta Maumivu Makali sana.
  • Kuganda kwa Damu panapo jitokeza Mgolo Hujaa na kuvimba sana na vimbe hii husababisha kuongezeka kwa maumivu..
  • Maumivi makali zaidi wakati wa kupata Haja Kubwa na wakati Mtu amekaa.
  • Hali hii ya kuganda kwa Damu ndani ya Mgolo inahitaji Matibabu ya Kitabibu.
WAKATI GANI UMUONE TABIBU
  • Pale Utakapoona kutokwa na Damu katika njia ya haja kubwa ijapokuwa kwa Mgolo ni kitu cha kawaida ila hunda kukawa na sababu nyingine zaidi zinazosababisha.
  • Pia  Uangalizi wa kitabibu na Matibabu ya haraka inapotokea Hali ya kutokwa Damu kwa Mtu anayetumia Dawa za kufanya wepesi wa Damu kitaalamu mfano  warfarin (Coumadin), clopidogrel (Plavix), or prasugrel (Effient) nk.
  • Mtu aliye na dalili nyingine mfano kichwa kuwa chepesi, kizunguzungu na udhaifu wa mwili huenda akawa amepoteza Damu zaidi na anahitaji Uangalizi wa haraka wa katabibu.
  • Mogolo huwa hausababishi maumivu ya Tumbo Lakini Hali hii ikijitokeza uanhitaji kumuona Tabibu mapema iwezekanavyo.
  • Mgolo Uliotoka nje ambao umehindikana kurudi ndani hata kwa kuurudisha taratibu unahitaji Uangalizi na Ushauri wa Kitabibu.
  • Mgolo wan je Uliopatwa na Mgando wa Damu waweza kuleta amumivu makali yanayohitaji Matibabu ya kitabibu Mapema.
MATIBABU YA MGOLO
     Matibabu binafsi Uwapo Nyumbani
      Maji ya Uvuguvugu
  • Kukalia Maji ya uvuguvugu kutwa Mara Tatu kwa muda wa Dakika 15-20 husaidia kupunguza Mgolo ulio vimba..
  • Ni muhimu kukausha vizuri eneo la haja kubwa baada kukalia maji ya uvuguvugu l kuepusha muwasho katika maeneo yanayozunguka eneo hilo.
Badilisha MLO

·         Vilainishi vya Choo Kikubwa
Vilainishi vya choo kikubwa husaidia kwa sehemu ijapokuwa choo kilaini sana husababisha vimbe ndani ya njia ya haja kubwa ama maambukizi. Ivyo ni vyema ukashauriana na Tabibu ama mfamasia wako.
     Mambo ya kuzingatia
  • Ni vyema mtu mwenye tatizo la mgolo kutokaa kitako kwa muda mrefu sana
  • Mazoezi ni muhimu sana naya msaada mkubwa katika kupunguza Hali ya Kupata Choo Kigumu na hivyo kupunguza Kani ya Mgandamizo ndani ya Hemorrhoidal Veins. Pia ni vizuri mtu kwenda Haja pale unapojisikia kufanya hivyo wala usijicheleweshe.
   


MTAZAMO JUU YA MADAWA
  • Dawa nyingi za kupaka na kuweka zilizo katika mifumo mbalimbali kama Gel, Creams, Ointments  na vidonge Husaidia kupunguza maumivu “Ijapokuwa” Haziponyeshi Mgolo, nyingi huwa na dawa zinazoweza kupunguza uvimbe na kujaa kwa Mgolo ama Mishipa inayovimba.

MATIBABU YA KITABIBU
Mgolo wa ndani uliotoka nje. (Prolapsed Internal Hemorrhoids)
  • Nyingi ya Migolo ya ndani inayotoka nje Hurudisha ndani kwa kuisukuma taratibu kupitia njia ya haja kubwa.
  • Kama Mgolo Utaendelea kubaki ukiwa umevimba na kujaa ukiwa nje ya njia ya haja kubwa na hakuna lakufanya katika hali kama hii njia za Upasuaji hutakiwa ili kuondoa Tatizo.
Mgolo Uliopatwa na Mgando wa Damu. (Thrombosed Hemorrhoids)
·         Mgolo wa nje uliopatwa na Mgando wa Damu (Thrombosed external haemorrhoids) unaweza kuleta maumivu Makali yanayoambatana na kitu kigumu katika eneo la haja kubwa na Haiwezekani kukisukuma ili kingie ndani. Mara nyingi Damu iliyoganda ndani ya Mgolo inahitaji kuondolewa kitaalamu kupitia Tabibu.
DONDO: Zipo aina ya Dawa ambazo endapo mtu atafuata Taratibu zinazotolewa hutibu Tatizo hili Moja kwa Moja, Dawa hizi zimetengenezwa ki-Asilia kutokana na Aina Fulani ya Mimea: Unaweza kuzipata kupitia Hapa Mydailyvalue
Jina la Dawa: Pilex Ointment and Pilex Tablet
Matumizi: Hutibu 1. Mgolo/ Mjiko ( hemorrhoids)
                              2. Hali ya Kuvimba Vena za Miguu (varicose veins)


·         Upasuaji (Surgery)

Kuna njia nyingi za upasuaji pale utakapoona Maumivu na kutoka Damu kusikokoma kwa muda Mrefu: kama unahitaji ushauri kutoka kwa wataalamu wetu ama kumwona Tabibu kwa ushauri na uchunguzi zaidi wasiliana nasi kupitia mydailyvalue

Jinsi ya kujikinga usipate Mgolo
Athali za kupatwa na Mgolo unaweza kuzipunguza kwa Kula Mlo /Chakula chenye Ufumwele wa kutosha, Kunywa Maji ya kutosha, Fanya Mazoezi Mara kwa Mara, jitahidi kwenda Haja kubwa Pale tu unapojisikia kufanya Hivyo.

No comments:

Post a Comment


widget